Wataalamu na maafisa watoa wito wa kuongezwa ushirikiano kati ya China na Ethiopia katika TVET

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Oktoba 24, 2023
Wataalamu na maafisa watoa wito wa kuongezwa ushirikiano kati ya China na Ethiopia katika TVET
Gong Zhiwu, Mkurugenzi Mkuu wa Muungano wa Elimu ya Ufundi wa China na Afrika, akizungumza kwenye semina ya ngazi ya juu kuhusu ushirikiano kati ya China na Afrika katika elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (TVET) mjini Addis Ababa, Ethiopia, Oktoba 22, 2023. (Xinhua/Michael Tewelde)

ADDIS ABABA - Wataalamu na watunga sera waliohudhuria semina ya ngazi ya juu kuhusu ushirikiano wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (TVET) kati ya China na Afrika wametoa wito wa kuimarisha uhusiano kati ya China na Ethiopia katika elimu ya TVET.

Semina ya Ushirikiano na Mabadilishano kitaaluma kuhusu TVET kati ya China na Afrika iliyofanyika Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, siku ya Jumapili iliwakutanisha maafisa waandamizi wa serikali ya Ethiopia, maafisa wa China, wasomi na wataalam, miongoni mwa wengine.

Kwenye semina hiyo, Teshale Berecha, Waziri wa Kazi na Ustadi wa Ethiopia, amesisitiza haja muhimu ya kuhimiza kufundishana na kushirikiana kwa pamoja kati ya Ethiopia na China katika nyanja ya TVET.

"Ushirikiano katika elimu ya TVET siyo tu ni jitihada za kitaaluma; ni daraja linalounganisha nchi zetu, kuongeza uelewa wa pamoja, na kuimarisha uhusiano unaotuunganisha pamoja," Berecha amesema.

Amesema Wizara ya Kazi na Ustadi ya Ethiopia "inasimama kama nguvu inayosukuma azimio letu la pamoja la kuimarisha ushirikiano katika nyanja ya TVET kati ya Ethiopia na China."

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Muungano wa Elimu ya Ufundi wa China na Afrika, Gong Zhiwu, amesema muungano huo umezindua miradi katika nchi kadhaa za Afrika, zikiwemo Ethiopia, Tanzania, Rwanda, Kenya, Uganda na Ushelisheli.

“Nchini Ethiopia, muungano umekuwa ukifanya kazi kwa karibu sana na Wizara ya Kazi na Ustadi ya Ethiopia juu ya mapitio ya pande zote na uboreshaji wa mfumo wa TVET nchini, ikiwa ni pamoja na sera na miongozo ya TVET, viwango vya kazi, mtaala, zana za tathmini, na ujenzi wa uwezo wa wafanyakazi na kitivo, uhusiano wa viwanda,” amesema Gong, huku akifafanua juu ya ushirikiano huo unaohusisha maeneo ya maendeleo ya viwanda, miundombinu ya kiuchumi, madini na uchimbaji, afya, kilimo, biashara, utamaduni wa michezo na utalii.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha

又大又粗又爽又黄的少妇_国产欧美日韩亚洲精品区_欧美重口另类在线播放二区_边做饭边被躁在线播放